Domcity Farming Center

Domcity Farming Center kufuga kuku kibiashara unatakiwa uwe na vitu vifuayavyo
AVAILABILITY, COMMITMENT, PASSION, LOCATION AND RESOURCES. Ushauri
Tupigie/WhatsApp 0656626173

Tujifunze Jambo Kupitia Mradi Wa AKM GLITTER Uliokusanya Vijana Kwaajili Ya Kujifunza Ufugaji Wa Kuku...✍️Mradi Ulijukan...
25/04/2026

Tujifunze Jambo Kupitia Mradi Wa AKM GLITTER Uliokusanya Vijana Kwaajili Ya Kujifunza Ufugaji Wa Kuku...

✍️Mradi Ulijukana Kwa Jina La TANGA YETU Kwasababu Huo Mradi Ulifanyikia MKOA WA TANGA...

🧲Wahenga Wanasema Ukistaajabu Ya Musa Utaona Ya Firauni Ndivyo Mambo Yanavyokwenda Hapa Duniani...

🧲🧲Mradi Ulikua Na Lengo Kuu Moja Kuwafundisha Vijana Buree Ili Wapate Ujuzi Wa Vitendo Namna Ya Kufuga Kuku Wakiamini Baada Ya Hayo Mafunzo Itawasaidia Kubadili Maisha Yao Kupitia Ufugaji Wa Kuku...

💥Mpango Kazi Ulipangwa Vizuri Kupitia Wataalam Mbalimbali Kwa Ufupi Mradi Ulikua Umejiandaa Vizuri Sana Kuliko Kawaida K**a Unavyoona Kwenye Picha Namna Ambavyo Mipango Ilivyopangika Vizuri...

💥💥Kikubwa Ninachotaka Kukujuza Ni Kwamba Mradi Ulikua Unahitaji Watu Wenye Kujitoa Kwamaana Hakuna Jambo Jepesi Kwenye Kufanikisha Kitu Chochote Duniani Ijapokua Utaandaliwa Kila Kitu Au Kupewa Kila Kitu...

🙄Kilichonishangaza Ni Kwamba Licha Ya Lengo Kuwa Zuri Ila Kuna Baadhi Ya Vijana Waliishia Njiani Yaani Hapo Ndipo Utaamini Mafanikio Sio Ya Kila Mtu...

🙄🙄Kumbuka Maandalizi Ya Mradi Ulifanywa Na Kampuni kuanzia UJENZI WA MABANDA,VIFAA VYA KUFUGIA,CHAKULA CHA KUKU,VIFARANGA,MADAWA NA HUDUMA ZOTE ZINAZOHITAJIKA KWENYE KUFANIKISHA ILO JAMBO YAANI HADI WATAALAM WALIKUWEPO KWENYE HUO MRADI...

🔥Hapo Ndipo Nikajifunza Kufanikiwa Inaanzia Moyoni Na Sio Kukurupuka Kwa Mihemko Naamini Kupitia Huo Mradi Wapo Walionufaika Na Kutumia Hayo Mafunzo K**a Sehemu Ya Kutengeneza Ajira Binafsi Ila Pia Wale Ambao Waliishia Njiani Naona Ufugaji Haukua Sehemu Ya Ndoto Zao Ila Waliingia Tu Kwasababu Ya Hamasa Ya Hayo Mafunzo...

🔥🔥Nenda YOU TUBE Andika TANGA YETU Utajifunza Namna Ambavyo Watu Wanaandaa Mradi Hadi Kufikia Malengo Husika Binafsi Hayo Mafunzo Niliyafatilia K**a Sehemu Ya Kunijenga Kimaarifa Na Wewe Unaweza Nufaika Pia...

NB;Nakala Hii Haipo Kwaajili Ya Kupromote Huo Mradi Maana Umefanyika Miaka 3 Iliyopita Lengo Langu Ni Ujifunze Kuwa Kufanikiwa Ni Moyo Na Sio Mihemko...

🏋️JITIHADA+🙏MAOMBI=MAFANIKIO💸👋Habari Ndugu,Natumaini Uko Salama Mzima Wa Afya Na K**a Haupo Sawa Nichukue Nafasi Hii Kuk...
17/04/2026

🏋️JITIHADA+🙏MAOMBI=MAFANIKIO💸

👋Habari Ndugu,Natumaini Uko Salama Mzima Wa Afya Na K**a Haupo Sawa Nichukue Nafasi Hii Kukuombea Upone Maradhi Uliyonayo Na MWENYEZI MUNGU Akufanyie Wepesi Kila Penye Uzito...

✍️Bila Kupoteza Muda Wako Twende Moja Kwa Moja Kwenye Mada Yetu Husika Ni Vipi JITIHADA Ukiambatanisha Na MAOMBI Matokeo Yake Ni Kufanikiwa...

💥Wengi Wetu Uwa Tunachanganya Sana Yaani Hatujui Namna JITIHADA Inavyofanya Kazi Kukupatia Mafanikio Na Pia Ni Jinsi Gani MAOMBI Yanaweza Kuwa Sehemu Ya Mafanikio Yako...

💥💥Ipo Hivi Ili Ufanikishe Jambo Lako Lolote Unatakiwa Kufanya JITIHADA Ya Mambo Yafuatayo...👇

1️⃣KUTAFUTA ELIMU YA KILE UNACHOTAKA KUKIFANYA...
..Jambo Lolote Iwe UFUGAJI Iwe BIASHARA Unapotaka Kuanza Ni Lazima Sio Hiari Utafute Maarifa Juu Ya Icho Kitu Ili Upate Urahisi Wa Kufanya Hilo Jambo Na Kupunguza Makosa Yenye Kurekebishika...
..Jamii Yetu Ya Sasa Tumekua Tukikurupukia Mambo Bila Kuwa Na Ujuzi Nayo Yaani Ukiwa Na Pesa Unakurupuka Kuanza UFUGAJI Au BIASHARA Kisha Baada Ya Kupata Hasara Au Ugumu Kwenye Hilo Jambo Lako Ndio Unaanza Kutafuta ELIMU Na Unakua Tayari Ushachelewa Maana Utakua Ushapoteza Pesa Yako Kwa Ukosefu Wa Maarifa...

✍️ Kwahiyo Tunatakiwa Kufanya JITIHADA Za Kutafuta Maarifa Juu Ya Jambo Lolote Tunalotaka Kulianza Hii Itatufanya Tufanikiwe Kwa Kiwango Kikubwa Yale Tunayoyaanza...

2️⃣KUANZA KWA MAJARIBIO ILI KUPIMA ELIMU ULIYONAYO KWA VITENDO...
..Baada Ya Kufanya JITIHADA Za Kutafuta ELIMU Jambo Linalofata Ni Wewe Kuanza Kwa Uchache Ili Kufanya Vipimo Vya ELIMU Uliyopata Ya Nadharia Uingize Kwenye VITENDO...
..Hapa Wengi Huwa Tunakua Na Pupa Ya Kuanza Kwa UKUBWA Sio Vibaya Ila Vizuri Zaidi Kuanza Kwa Uchache Ili Ukue Kulingana Na Picha Utakayoipata Yaani Ata Mbuyu Ulianza Kwa Kuota Mbegu Sio K**a Ulikua Tu Mkubwa Tu K**a Unavyouona...
..Kila Jambo Lina Hatua Zake Ndio Maana Ata Mtoto Anahatua Zake Za Ukuaji K**a Vile Anaanza Kujifunza Kukaa,Kisha Kusimamia Vitu,Kisha Kunyanyua Mguu Na Hatimae Anaanza Kupiga Hatua Ndivyo Inavyotakiwa Kwenye Jambo Lolote Unapoanza Lipe Muda Wa Ukuaji Usifanye Mambo Kwa MIHEMKO...

✍️ kwahiyo Tujitahidi Kufanya Vitu Kwa Taratibu Tupunguze MIHEMKO Ambayo Huwa Inatupelekea Kuishia Njiani...

3️⃣UVUMILIVU NA SUBRA PALE UNAPOKUMBANA NA CHANGAMOTO...
..Hapa Ndio Jamii Yetu Inapoamini Mafanikio Sio Kwaajili Ya Kila Mtu Maana Hakuna Jambo Linalohitaji JITIHADA Kubwa K**a Kukabaliana Na Changamoto...
..Je Ukijipima Unahuo Ubavu Wa Kuvumilia Au Ndio Unaamini Unapotaka Jambo Lako Kutimia Hautaki Kukumbana Na Vikwazo...
..K**a Unahitaji Kujitofautisha Na Watu Waliolishindwa Jitengenezee Nguvu Ya JITIHADA Ya Kukubali Na Kuzipokea Changamoto Na Kuendelea Na Safari Ukiweza Kuvuka Hii Hatua Utakuja Kutoa Ushuhuda Mbele Ya Safari Tupo Hapaa...

✍️ Kwahiyo Kumbuka Hakuna Mafanikio Yasiokua Na Changamoto Na Vikwazo Ukiona Mtu Anafurahia Ushindi Jua Kapitia Mapito Ya Kukatisha TAMAA Mpaka Kufikia Hapo Alipo...

🙏🙏MAOMBI🙏🙏..HAPA TUNAFUPISHA KWA KUSEMA MTU ANAYEFANYA MAMBO YAKE AKIWA NA IMANI YA KUMTEGEMEA MWENYEZI MUNGU MARA ZOTE YUPO TAYARI KUMSHUKURU MOLA WAKE KWA KILA HATUA ANAYOIPITIA KWAHIYO INAMFANYA AWE NA NGUVU ZA KIMWILI NA KIROHO KUFIKIA MAFANIKIO AMBAYO WENGINE HAWAWEZI KUFIKA NA KUISHIA NJIANI...

💕Naamini Umejifunza Jambo NAKUPENDA SANA NA PIA NAKUTAKIA MAFANIKIO MEMA KATIKA HARAKATI ZAKO TUSEME AMINA🙏

🙆TUNASHINDWA KUANZA KWASABABU TUNATAKA KUANZA KWA UKUBWA...💣Hiki Kifungo Cha Kutoanza Jambo Kwasababu Fikra Na Mawazo Ye...
11/04/2026

🙆TUNASHINDWA KUANZA KWASABABU TUNATAKA KUANZA KWA UKUBWA...
💣Hiki Kifungo Cha Kutoanza Jambo Kwasababu Fikra Na Mawazo Yetu Yanatuambia Kwamba Muda Wa Kuanza Bado Tusubiri Tuwe Na Mtaji Mkubwa Ndio Tuanze Ni Bomu Ambalo Tunalitengeneza Wenyewe Na Linatuangamiza Wenyewe...

✍️Ipo Hivi Tunaweza Kuwa Na Maono Makubwa Kuhusu Jambo Fulani Mfano....👇

"Mtu Anataka Kuanza Ufugaji Wa Kuku Ila Picha Aliyonayo Kichwani Ni Kwamba Mimi Siwezi Nikaanza Ufugaji Kwa Kuku Wachache Nataka Nikianza Nianze Na Kuku Wengi Ili Nipate Faida Kubwa..."

"Mtu Anataka Kuanza Biashara Ila Maono Aliyonayo Ni Kwamba Nataka Nikianza Nianze Na Mzigo Mkubwa Yaani K**a Ni Duka La Nafaka Basi Niwe Na Nafaka Zote Dukani Ili Mteja Akija Asikose Bidhaa Yoyote..."

✍️Amini Kwamba Mawazo Au Fikra Au Maono Yakutaka Kufanya Vitu Kwa Ukubwa Sio Mabaya Ila Ubaya Unakuja Pale Unapotaka Kuanza Halafu Hizo Fikra Ndio Zinakua Kipaumbele Chako Yaani Lazima Nianze Kwa Ukubwa Sitaki Mchezo Mimi Kinyume Na Hapo Bora Nisianze...

🛑Fikra Hizi Zinaweza Zikawa Sahihi Kwako Endapo Tu Ushawahi Kufanya Hiyo Biashara Au Huo Ufugaji Kwahiyo Ushajua Mbivu Na Mbichi...
Yaani Nikiwa Na Maana Unaingia Kwaajili Ya Kuendeleza Kile Unachokifahamu Kivitendo Na Sio Kimawazo...

🛑🛑Ila K**a Haujawahi Kufanya Hiyo Biashara Au Huo Ufugaji Ndio Kwanza Unataka Kuanza Mara Ya Kwanza Basi Fikra Hizo Hazitakua Sahihi Kwasababu Zifuatazo...👇

1️⃣KUANZA KWA UKUBWA SIO SABABU YA KUFANIKIWA K**A TUNAVYOFIKRIA...
..Hii Dhana Ya Kuanza Kwa Ukubwa Tukiamini Ndio Sababu Ya Kufanikiwa Zaidi Ni Dhana Mbaya Sana Na Imepelekea Watu Wengi Kupata Anguko Takatifu Na Kusababisha Kupoteza Mitaji Yao Walioitafuta Kwa Tabu Sana...

👉Ipo Hivi Tunaingia Kwenye Utekelezaji Wa Jambo Tukiwa Na Picha Ya Mafanikio Ila Pindi Tutakapoanza Tunakutana Na Uhalisia Ambao Hatukuhujua Wala Kuufikiria Kabla K**a Inaweza Kuwa Hivyo Mfano...👇

"Umeanza UFUGAJI WA KUKU Kwa Idadi Kubwa Ila Haujawahi Kufuga Kabla Ndio Unaanza Kwa Mara Ya Kwanza Kwahiyo Hauna Ukomavu Au Ubobezi Wa Kivitendo Kwenye Hilo Jambo...
..Utakapoingia Utakutana Na Uhalisia Wa Changamoto Za Ufugaji K**a Vile Vifaranga Kufa, Changamoto Ya Mgonjwa Au Kukutana Na Gharama Ambazo Ulikua Hauzijui K**a Zipo Kwenye Hiyo Safari Yako Ya Ufugaji...
..Hapo Ndio Unapokuta Watu Wanapoteza Pesa Zao Kwasababu Ya Matarajio Kwenda Kinyume Na Matakwa Yao Kwasababu Tu Waliamini Mtaji Mkubwa Ndio Kufanikiwa...

2️⃣PESA SIO KILA KITU...
..Hapa Ndio Tunarudi Na Kukumbuka Midahalo Ya Shuleni Kwamba "PESA NI BORA KULIKO ELIMU AU ELIMU NI BORA KULIKO PESA..."
..Sina Nia Ya Kuweka Mjadala Kuhusiana Na Ukinzani Wa Uelewa Kuhusu Hivyo Vitu Viwili Kipi Kinamtangulia Mwenzake Yaani PESA VS ELIMU...
..Ila Watu Wengi Wamejikuta Wanatumbukia Kwenye Biashara Au Ufugaji Kwa Kuamini Nikianza Na Mtaji Mkubwa Ndio Kufanikisha Jambo Langu Huku Akiwa Na Imani Pesa Ndio Silaha Ya Mafanikio Yake...
..Jambo Ambalo Limepelekea Watu Kupoteza Mitaji Yao Kwasababu Waliingia Kwenye Jambo Ambalo Hawana ELIMU Nalo Na K**a Elimu Waliokua Nayo Ni Ile Ya Nadharia Na Hawakupata Nafasi Ya Kufanya Kimatendo...
..Mwishowe Watu Wamejikuta Wanapoteza Pesa Na Muda Wao Mfano...👇

👉 Mtu Kafungua Duka La Nguo Za Watoto Na Kwakua Anaamini Kuanza Kwa Ukubwa Ndio Kufanikiwa Kwake Akajaza Nguo Za Watoto Kulingana Na Fikra Na Maono Yake...
Baada Ya Kuanza Biashara Anajikuta Nguo Alizonunua Sio Zinazotoka Sana Na Zile Zinazofanya Vizuri Sokoni Kaziweka Chache Sana...
Je...!!! Mtu Huyu Anaweza Endelea Na Hiyo Biashara Wakati Kodi Na Mshahara Wa Mfanyakazi Wake Vinahitajika Na Mzunguko Wa Biashara Umekua Mdogo Kwake...???
..Kwahiyo Mtu Wa Namna Hii Utamkuta Anakuja Kuijua Biashara Akiwa Tayari Ameshawekeza Pesa Nyingi Ambazo Zinaenda Kuteketea Kwa MIHEMKO Ya Kuanza Jambo Kwa Ukubwa Bila Kua Na Uzoefu Wa Hiyo Biashara...

🙆🙆Tuelewane Jambo Moja Sio Kwamba Mtu Yoyote Anayeanza Moja Kwa Moja Kwa Mtaji Mkubwa Lazima Ataanguka Hapana Ila Ni Muhimu Zaidi Kuanza Kidogo Kidogo Ili Utambue Kwa Kina Kile Unachokifanya Baada Ya Hapo Ndio Uweke NGUVU ZAIDI Baada Ya Kujiridhisha Kivitendo...

💁💁 Kwahiyo Nitoe Rai Kwako Msomaji Pendelea Zaidi Kuanza Kidogo Kidogo Ili Ukikua Ukue Jumla Kuliko Kuwaza Kuanza Kwa Ukubwa Ambao Unaweza Kukukatisha TAMAA Endapo Utapata Anguko Kumbuka Hizi Ni Biashara Na Changamoto Ni Sehemu Ya Maisha Ya Biashara...

✍️Sio Lazima Kujichelewesha Kuanza Mpaka Uwe Na Mtaji Mkubwa Anza Sasa Ili Ukue Taratibu Na Naamini KWA UWEZO WAKE MOLA UTAFIKA HUKO UNAPOTAKA...

🙏🙏...MOLA AKUBARIKI KATIKA SAFARI YAKO YA UPAMBANAJI...🙏🙏

🤷JE..!!! NI KWELI KILA MTU ANAWEZA KUWA MFUGAJI WA KUKU...?🐓?🐓?👋Hello Ndugu Zangu Ni Muda Umepita Ila Naamini Mpo Wazima...
10/04/2026

🤷JE..!!! NI KWELI KILA MTU ANAWEZA KUWA MFUGAJI WA KUKU...?🐓?🐓?

👋Hello Ndugu Zangu Ni Muda Umepita Ila Naamini Mpo Wazima Bila Kupoteza Muda Twende Kwenye Mada Husika K**a Inavyojieleza Hapo Juu...👉"NI KWELI KILA MTU ANAWEZA KUWA MFUGAJI WA KUKU...???

🗣️Unaweza Ukawaza Na Kuwazua Ukahisi Majibu Ni Mepesi K**a Unavyofikiria Yaani Kujibu NDIO AU HAPANA Ni Jambo Jepesi Ila Kuelezea Kwanini NDIO AU HAPANA Hapo Ndio Sehemu Muhimu Ambayo Kila Mmoja Wetu Anatamani Kujua. Ila Usijali Tupo Hapa Kufundishana Na Kuelimishana Kwa Hoja Zikiambatana Na Mantiki...✍️

🌍Duniani Kila Mtu Amekuja Akiwa Na KUSUDI Lake Kupitia Hilo KUSUDI Ndani Yake Unakutana Na Kipaji Yaani Unafanya Jambo Bila Kutumia AKILI NYINGI Au NGUVU NYINGI Kulifanikisha...

"Mfano 1️⃣ Darasani(SHULENI) Kuna Watu Walikua Wanafaulu Sana Mitihani Ila Hao Hao Wanaofanya Vizuri Darasani Wakienda Kwenye Mpira Unakuta Wanazidiwa Na Wale Watu Wasiofanya Vizuri Darasani..."

"Mfano 2️⃣ Kuna Baaadhi Ya Watu Wanafanya Vizuri Sana Kwenye Ufugaji Ila Hawajasomea Ufugaji Yaani Hawajaenda Chuo Kusomea Mambo Ya Mifugo Na Wakati Huo Huo Kuna Watu Wamesomea Mambo Ya Mifugo Ila Akifanya Ufugaji Hapati Matokeo Makubwa K**a Wengine Licha Ya Kusomea Hiyo Elimu..."

📌 Naomba Nikuulize Swali Ila Lijibu Kichwani Mwako Kisha Tuendelee Na Mada Yetu...👇

JE...!!! UNAAMINI DUNIANI KILA MTU AMEKUJA AKIWA NA KUSUDI MAALUMU NDANI YAKE...???

👉 Nashukuru Kwa Kulijibu Swali Letu Ayaa Tuendelee 🤗...
Kwahiyo Ukitazama Jamii Yetu Ya Sasa Kutokana Na Changamoto Za Kimaisha Imepelekea Watu Wengi Kukimbilia UFUGAJI WA KUKU Wakiamini Ni Jambo Jepesi Ambalo Kila Mmoja Anaweza Kulifanya Na Kufanikiwa...

🔥Baada Ya Hiyo MITAZAMO Ya Kuamini UFUGAJI WA KUKU Ni Jambo Jepesi Na Rahisi Kukuletea Mafanikio Imesababisha Watu Wengi Kukutana Na Changamoto Nyingi Ikiwemo...👇

💰💸 KUPOTEZA MITAJI YAO WALIOKUA WANAITEGEMEA KWA MAMBO MENGINE...

🐔🐤 KUPOTEZA KUKU KWA VIFO VISIVYOKUA NA MAJIBU...

🙆🙆 KUKATAA TAMAA NA UFUGAJI NA KUPELEKEA MABANDA KUBAKI K**A MAGHOFU YASIO NA KAZI TENA...

🤷🤷KUAMINI KWAMBA MANENO YASEMWAYO KUKU ANAWEZA KUKUKOMBOA KIMAISHA NI PROPAGANDA YAANI SIO KWELI...

🛑Binafsi Naamini Kufanikiwa Au Kutofanikiwa Kwenye UFUGAJI WA KUKU Inategemea Na Utayari Wako Na Namna Gani Umejiandaa Kukabaliana Na Kila Matokeo Yatakayojitokeza...

"Yaani K**a Umeingia Kwenye UFUGAJI Kwa Lengo La Kutafuta Pesa Na Sio Kwa Mapenzi Ya UFUGAJI Ni Ngumu Kudumu Na Kufikia Malengo Uliyokusudia..."

🙆🤷Usichanganyikiwe Twende Taratibu Tutaelewana Tu😂... Ipo Hivi Kuna Makundi Matatu Ya Watu Wanaoingia Kwenye UFUGAJI Ambayo Ni...

1️⃣MTU ANAYEPENDA KUTOKA MOYONI...
..Hili Ni Kundi La Watu Ambao Wao UFUGAJI Upo Damuni Yaani Yeye Anaamini Mafanikio Yake Hapa Duniani Yapo Kwenye UFUGAJI Na Sio Kitu Kingine Chochote Na Mara Nyingi Watu Hawa Ndani Yao Utakutana Na KUSUDI LA UFUGAJI Yaani Wamekuja Duniani Kwaajili Ya Kufanya Hiyo Kazi Kwahiyo Ukikutana Na Mtu Wa Namna Hii Umwambii Chochote Akakuelewa Yaani Bora KUKU Wafe Na Afuge Tena Ila Sio Kuacha UFUGAJI...

2️⃣MTU ALIYEONA FURSA KWENYE UFUGAJI...
..Hili Ni Kundi La Watu Ambao Wao UFUGAJI Sio KUSUDI Lao Ila Wameona FURSA Kwenye UFUGAJI. Watu Hawa Huwa Wanafanya UFUGAJI K**a Daraja La Kuwavusha Kwenda Kwenye KUSUDI Lao Na Mara Nyingi Utakuta Anapambana Na Unaona Kabisa Anafanya Vizuri Ila Baada Ya Muda Utamkuta Ameachana Na UFUGAJI Yupo Kwenye Mambo Yake Mengine. Unaweza Baki Na Mashangao Kwanini Ameacha Kufuga...!!!
Ila Pia Kundi Ili Mara Nyingi Uishia Njiani Wakiona Kile Walichokua Wanakitafuta Wamekikosa Na Wanarudi Kwenye KUSUDI Lao Waliloliacha...

3️⃣MTU ANAYEFUGA KWA MIHEMKO AU STORI ZA MTANDAONI...
..Hawa Ndio Wenzangu Na Mimi Yaani Tumeingia Kwenye UFUGAJI Kwasababu Tu Yakusikia Au Kuona Fulani Amefanikiwa Kupitia KUKU Ngoja Na Mimi Nifuge...😀
Kundi Ili Lawama Na Malalamiko Huwa Ni Mengi Sana Na Usipokua Makini Anaweza Kukukatisha TAMAA Kwasababu Ya Kushindwa Kwake...
👉Kundi Ili Uwa Halijifichi We Pitia Comment Utaona Namna Wanavyochangia Utajua Tu Huyu Sio MFUGAJI Ila Yupo Tu Kwasababu Ya MIHEMKO...

📚Nafunga Kikao Chetu Kwa Kusema Kuwa Asilimia Kubwa Za Kufanikiwa Zipo Kwa Yule Ambaye UFUGAJI WA KUKU NI KUSUDI Lake...

Ila Pia Wale Ambao Sio KUSUDI Ila Wanaingia Kwenye UFUGAJI Kwasababu Wanamapenzi Na UFUGAJI Na Wao Wanaasilimia Kubwa Ya Kufanikiwa...

NB: UKIJIONA UNAINGIA KWENYE UFUGAJI KWA TAMAA NA MIHEMKO BORA UTAFUTE KAZI NYINGINE YA KUFANYA...

🙏MOLA AKUBARIKI KWA KUSOMA BILA KUCHOKA NIMEREJEA KWA NGUVU YA 10G TUPO PAMOJA...✍️

Address

Dom Town
Dodoma

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Domcity Farming Center posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share

Category