05/08/2026
Mmetoa formula ya chakula kwa vifaranga 100 mimi nataka kuingiza vifaranga 150 nifanyaje
MAJIBU ๐๐ฝ๐๐ฝ๐๐ฝ๐๐ฝ
Nafikiri unamaanisha kuwa tumetoa formula ya chakula vifaranga kwa kiwango cha kilo 100
Kiwango hiki Cha chakula kilo 100 kinatosha kwa vifaranga 100 kuanzia siku 1 mpaka siku 25 sawa sawa na maelekezo yetu
K**a wewe ni mgeni, maelezo yetu ni kuwa kifaranga mmoja anakula chakula kilo 1 kuanzia siku 1 mpaka siku 25 maana yake vifaranga 100 watakula chakula kilo 100 kwa siku 25 yaani kuanzia siku 1 mpaka siku 25
Kwa vifaranga 150 unahitaji chakula kilo 150 kwahiyo unapochanganya utaweka hivi ๐๐ฝ
Mahindi kilo 78
Soya kavu kilo 48
Mashudu ya alizeti kilo 13.5
Mafuta ya mboga kilo 3[Lita 2.7]
CFP ya vifaranga kilo 7.5
Jumla kilo 150
Kwa Arusha CFP zinapatikana kwa wakala wetu namba zake hizi hapa ๐๐๐๐ ๐๐๐ ๐๐๐
Pia wakala ana mizani, thermometer na cup ni***es.