Moshi Agrovet

Moshi Agrovet Tunauza CFP,vifaa vya kuku, chanjo,dawa na vitamini za kuku. Hatuuzi vifaranga โŒ

Mmetoa formula ya chakula kwa vifaranga 100 mimi nataka kuingiza vifaranga 150 nifanyaje MAJIBU ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐ŸฝNafikiri unamaan...
05/08/2026

Mmetoa formula ya chakula kwa vifaranga 100 mimi nataka kuingiza vifaranga 150 nifanyaje

MAJIBU ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ

Nafikiri unamaanisha kuwa tumetoa formula ya chakula vifaranga kwa kiwango cha kilo 100

Kiwango hiki Cha chakula kilo 100 kinatosha kwa vifaranga 100 kuanzia siku 1 mpaka siku 25 sawa sawa na maelekezo yetu

K**a wewe ni mgeni, maelezo yetu ni kuwa kifaranga mmoja anakula chakula kilo 1 kuanzia siku 1 mpaka siku 25 maana yake vifaranga 100 watakula chakula kilo 100 kwa siku 25 yaani kuanzia siku 1 mpaka siku 25

Kwa vifaranga 150 unahitaji chakula kilo 150 kwahiyo unapochanganya utaweka hivi ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ

Mahindi kilo 78
Soya kavu kilo 48
Mashudu ya alizeti kilo 13.5
Mafuta ya mboga kilo 3[Lita 2.7]
CFP ya vifaranga kilo 7.5

Jumla kilo 150

Kwa Arusha CFP zinapatikana kwa wakala wetu namba zake hizi hapa ๐ŸŽ๐Ÿ•๐Ÿ—๐ŸŽ ๐Ÿ•๐Ÿ—๐Ÿ— ๐Ÿ•๐Ÿ”๐Ÿ”

Pia wakala ana mizani, thermometer na cup ni***es.

Umuhimu wa nafasi na vyombo vya chakula na maji katika ukuaji wa kuku 1.Nafasi sahihi ni muhimu k**a unataka kuku wako w...
05/08/2026

Umuhimu wa nafasi na vyombo vya chakula na maji katika ukuaji wa kuku

1.Nafasi sahihi ni muhimu k**a unataka kuku wako wakue vizuri

Ukiwabananisha kuku wako hawatakua vizuri, vifaranga wanahitaji eneo dogo ukilinganisha na kuku wakubwa hivyo kuku wanavyokua inabidi utanue bruda yako kwa kawaida siku 5-7 inatakiwa utanue bruda na Utaendelea kuitanua kila wiki

Kwa kuku chotara wakubwa (kuanzia wiki 3) wanakaa kuku 10 kwenye skwea mita moja (urefu zidisha upana)

Maana yake kwa mfano wetu wa kuku chotara 200 unahitaji Banda la skwea mita 20 ambalo linaweza kuwa urefu Mita 5 upana mita 4 au urefu Mita 10 upana mita 2

200/10=10

Nimeona wafugaji baadhi wanajenga Banda la kutoshea kuku 300 (skwea mita 30) ila anaweka kuku 500 baadae analalamika kuku hawakui ๐Ÿคท๐Ÿฝโ€โ™‚๏ธ

Hivyo Jenga Banda SAHIHI kulingana na idadi ya kuku unaotaka kuwafuga

2.Vyombo vya chakula na maji

Unaweza kuwa na Banda SAHIHI ila ukaweka vyombo vichache kuku wako hawatakua vizuri

Mf Una kuku 200 nafasi kwenye banda iko sawa ila umeweka vyombo vya chakula 3 na vya maji 2 hili ni tatizo kivipi?

Fikiria kuku 200 inabidi wale kwenye vyombo vya chakula 3 unajua ushindani wake ni zaidi ya ligi ya mabingwa na wale wababe ndio watakaokula chakula maana yake utakuwa na non uniformity ya hatari

Yaani kuku watapishana sana utakuwa na kuku wakubwa wachache na wadogo wengi sana

Kumbuka unapopokea vifaranga huwa hawana uzito unaofanana, kuna wakubwa na wadogo tokea siku ya kwanza

Sasa ukiweka vyombo kwa idadi sahihi inasaidia kupunguza non uniformity/kuku kupishana ukubwa (umbo/uzito)

Hivyo weka

1.Feed Moja (chombo cha Chakula) cha kuanzia kilo 3 kwa kuku 20-25 hivyo kwa kuku 200 uwe na walau vyombo vya chakula 8-10

Feed Moja ya kilo 3 ni sh 6000

2.Vyombo vya maji

Weka drinker moja ya Lita 10 kwa kuku 50 maana yake kwa kuku 200 unahitaji drinker 4 za Lita 10

Drinker moja ya Lita 10 ni 10,000

Ukizingatia hayo na kuwapa kuku wako chakula Bora kwa kutumia CFP kuku wako watakua vizuri sana na utawauza mapema๐Ÿ”ฅ

Sisi Hatuuzi vifaranga, Tunauza CFP, soya kavu, dawa , chanjo, vitamin na vifaa vya ufugaji wa kuku Hakuna mahali popote...
30/07/2026

Sisi Hatuuzi vifaranga, Tunauza CFP, soya kavu, dawa , chanjo, vitamin na vifaa vya ufugaji wa kuku

Hakuna mahali popote tumesema tunauza vifaranga

Tafadhali soma ujumbe ujue tumekusudia nini usiangalie picha na kutengeneza mtazamo wako bila kusoma ujumbe !

Je CFP ni nini ? Kirefu chake ni nini?

Kirefu chake ni chotara feed pack...

CFP ni virutubisho vinavyotumika kuandaa chakula cha kuku chotara kuanzia siku 1 mpaka unapowauza au wanapoanza kutaga

Ukiwa na CFP unahitaji pumba za mahindi, mashudu ya alizeti, mahindi, mafuta na soya au dagaa kukamilisha chakula cha kuku wako.

Nikupe mfano wa chakula cha vifaranga kilo 100 kwa formula yenye mafuta ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ

Mahindi kilo 52
Soya kavu kilo 32
Mashudu ya alizeti kilo 9
Mafuta ya mboga kilo 2 [ Lita 2.26]
CFP ya vifaranga kilo 5

Jumla kilo 100

Ukitumia CFP huhitaji kuweka vitu vidogo k**a dcp, chokaa, premix,chumvi, Toxibinder kwasababu vitu hivyo vyote vipo ndani ya CFP

Rahisisha uchanganyaji wa chakula cha kuku wako kwa kutumia CFP

Tunapatikana Dodoma Majengo Sokoni
Mawasiliano 0752 912132 au 0718 192 378

1.Je CFP ni kwa ajili ya chotara aina gani?2.Nina kuku wa mayai je naweza kutumia CFP kuwatengenezea chakula ?MAJIBU ๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡...
29/07/2026

1.Je CFP ni kwa ajili ya chotara aina gani?

2.Nina kuku wa mayai je naweza kutumia CFP kuwatengenezea chakula ?

MAJIBU ๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡

1.CFP inatumika kwa Chotara aina zote na kuku wa kienyeji iwe Tanbro, sasso, kuroiler, chotara wa mchina na aina nyingine pamoja na kienyeji.

2.Unaweza kutumia CFP kuwatengenezea chakula kuku wa mayai kwa kutumia CFP

Endelea kufuatilia page yetu kujifunza zaidi kuhusu ulishaji wa kuku kwa kutumia CFP

Kwa Arusha CFP zinapatikana kwa wakala wetu namba zake hizi hapa ๐ŸŽ๐Ÿ•๐Ÿ—๐ŸŽ ๐Ÿ•๐Ÿ—๐Ÿ— ๐Ÿ•๐Ÿ”๐Ÿ”

Pia wakala ana mizani, thermometer na cup ni***es.

Mkuu samahani kuku anaetaga ndio mwnye uwezo wa kula gram 120 Kwa siku Hawa chotara na broiler hesabu Yao Ni kilo 2 mpka...
29/07/2026

Mkuu samahani kuku anaetaga ndio mwnye uwezo wa kula gram 120 Kwa siku
Hawa chotara na broiler hesabu Yao
Ni kilo 2 mpka 3 Kuanzia day 1 mpka siku 30-35

MAJIBU ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ

Kumekuwepo na hoja nyingi kujibu moja ya post yetu kuwa chotara 500 wenye umri wa siku 35 watakula chakula kilo 70 sawa na gram 140 kwa kuku mmoja

Hoja mojawapo ndio hii hapa kuwa kuku wanaotaga ndio wanaweza kula gram 120, kwa layers ni sahihi wanakula gram 110-120 kutegemeana na mfumo wa ufugaji na mazingira

Sasa Hapa tunaongelea chotara sio layers

Kuna chati tumeitoa sijui k**a mmeifuatilia ila kukutofautishia tu ili upate picha chotara mmoja wa siku 28 anakula gram 101 kwa siku wakati layers wa wiki 18 ndio anakula gram 100 ๐Ÿ˜ณ๐ŸŽฏ

Fanya mambo haya Kujifunza zaidi...

1.Kwanza pakua hii chati ya kuku wa sasso ambayo utaitumia kujua kiwango cha chakula wanachokula kila siku kuanzia siku 1 mpaka siku 60

Kupakua hiyo chati bofya hii link hapa๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ

https://drive.google.com/file/d/1JyGNxKDUKYsQyaQAkHvE0KB-702M1Mhr/view?usp=drivesdk

๐Ÿ‘‰๐ŸฝK**a huwezi kupakua hii chati tafuta mtu akusaidie kuipakua na unaweza kwenda nayo stationery wakakuchapishia ukawa na nakala ngumu [hard copy]

๐Ÿ‘‰๐ŸฝChati hii ni ya sasso na tunaitumia kwa kuku chotara aina zote, hatuna chati za chotara wengine k**a unayo unaweza kuitumia.

2.Jambo la pili Jifunze kutumia hiyo chati kwa kuangalia hii video hapa kwa kubofya hii link ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ

https://youtu.be/ssrq3vHNL0o

๐Ÿ‘‰๐ŸฝK**a unapata changamoto kuangalia hii video tafuta mtu akusaidie namna ya kufungua hii video ya YouTube najua tunatofautiana!

3.Jambo la tatu hakikisha unawalisha kuku kwa kipimo kila siku k**a ambavyo hiyo chati inaonesha kiwango husika kwa kila siku

Hapa unahitaji mzani, k**a Bado huna mzani tupigie 0752 912132 kuagiza mzani wa kidijitali bei yake ni 20,000 na unapima kuanzia gram 100 mpaka kilo 50. Pia unaweza kufika ofisini kwetu Moshi Agrovet tunapatikana Dodoma Majengo Sokoni

Zingatia kwamba kiwango cha chakula wanachokula kitakuwa kinabadilika kadri wanavyokua siku kwa siku

4.Ulishaji wa chakula ni asubuhi na mchana utagawa chakula nusu kwa nusu yaani k**a kuku wako chotara wanakula chakula kilo 20 kwa siku utawapa kilo 10 asubuhi na jioni utawapa kilo 10

๐€๐๐†๐€๐‹๐ˆ๐™๐Ž

Jifunze jinsi ya kuwalisha kuku wako kwa kufuata viwango vinavyoelekezwa kupitia hiyo chati

Tafadhali sisi hatutakufanyia hayo mahesabu ndio maana tumeandaa chati na hiyo video ili uweze kujifunza na kufanya wewe mwenyewe kila siku hapo bandani kwako.

Ni rahisi Wala sio ngumu

Asante sana kwa usikivu wako kwenye hili suala ๐Ÿ™๐Ÿฟ

CFP
Ulishaji wa uhakika

"Kuku waliomaliza starter mapema gharama yao mpaka tunamaliza kuwauza Imekuwa ndogo kuliko ambao waliochelewa kumaliza s...
27/07/2026

"Kuku waliomaliza starter mapema gharama yao mpaka tunamaliza kuwauza Imekuwa ndogo kuliko ambao waliochelewa kumaliza starter"

Majibu๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ

Mdogo wangu aliniambia hii kauli baada ya kulinganisha ukuaji na gharama ya batch mbili Kuna batch moja vifaranga walikuwa vizuri kwenye ulaji wa chakula na batch nyingine tulipata ina changamoto balaa ulaji wao ulikuwa chini sana

Mwanzoni mdogo wangu alikuwa anafikiria k**a wafugaji wengine kuwa vifaranga wakichelewa kumaliza stata ni nzuri kwasababu kile chakula kinakuwa kimesogeza siku

Nikupe mfano katika mfumo wetu wa ulishaji tunawapa vifaranga stata kuanzia siku 1 mpaka siku 25, wakati mwingine vifaranga wanamaliza stata mapema labda siku 23, 24 au 25 na wengine ubora ukiwa chini wanachelewa kumaliza stata mpaka siku 28 au 30!

Wafugaji wengi huwa wanapata shida wakiona ulaji wa vifaranga Uko juu na vifaranga wanamaliza chakula mapema

Sasa Baada ya kijana kupiga hesabu ndio akanitumia huo ujumbe, nilimwambia apige hesabu za gharama ya chakula kwa batch zote mbili - waliomaliza stata mapema na waliochelewa mpaka wanauzwa!

Baada ya muda alinirudia na hili jibu๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ

"Kuku waliomaliza starter mapema gharama yao mpaka tunamaliza kuwauza Imekuwa ndogo kuliko ambao waliochelewa kumaliza starter"

Yesssssss

Hii ni sahihi kwasababu vifaranga wakiwa wadogo wanakuwa wanahitaji chakula kidogo ili waweze kukua

Kadri kuku wanavyokua wanahitaji chakula kingi zaidi kukupa uzito

Kifaranga anatumia chakula kingi anachokula kwa ajili ya ukuaji [growth] wakati kuku mkubwa anatumia chakula kingi kufanya maintenance kuliko ukuaji

Unaweza kujifunza zaidi kuhusu hili kwa kusoma kuhusu "FEED CONVERSION RATIO" - FCR

Kiufupi vifaranga wakimaliza stata mapema ni habari njema FURAHI

Vifaranga wakiwa na ulaji mzuri wa chakula FURAHI

Naomba kuuliza kiongoz samahan Kwa uvamizi, kunakitu hamjafafanua pale kwenye group.Kuku mmoja kuanzia siku 25 Hadi 60 a...
27/07/2026

Naomba kuuliza kiongoz samahan Kwa uvamizi, kunakitu hamjafafanua pale kwenye group.
Kuku mmoja kuanzia siku 25 Hadi 60 anakula jumla ya kilo 4.5
Je kiasi hiki atakula ukimlisha usiku na mchana au ni mchana pekee?
Je akitimiza miezi miwili atakua na uzito gani?
Chotara wa miezi miwili bei yake sokoni ni shngap?

๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ

1.Kuku mmoja kuanzia siku 25 Hadi 60 anakula jumla ya kilo 4.5
Je kiasi hiki atakula ukimlisha usiku na mchana au ni mchana pekee?

๐Ÿ‘‰๐Ÿฝ Watakula usiku na mchana Utawapa chakula asubuhi na jioni

๐Ÿ‘‰๐ŸฝK**a una mzani unaweza kupima ili kujua kiwango cha Chakula wanachokula mf kuku 500 umri wao siku 35 kwa siku wape kilo 70 [sawa na kuku mmoja anakula gram 140]

Saa 1 Asubuhi unawapa kilo 40 na Saa 10/11 jioni wape kilo 30

Usiku hatuwazimii taa

Uwiano wa gram 140 kwa kuku utakupa matokeo mazuri kuliko ukiwapa Chini ya hapo

Utakapoanza kuwachanganyia chakula (siku 25) kuku 500 hawawezi kula kilo 70 kwa siku, unaanza kuwapa kilo 40, ukiona wanamaliza unaongeza unawapa kilo 50 hivyo mpaka kufikia siku 35-38 wanakuwa wanamaliza kilo 70 na Utaendelea na kiwango hicho mpaka uanze kuwauza

2.Je akitimiza miezi miwili atakua na uzito gani?

๐Ÿ‘‰๐ŸฝKilo 1.5-2.2, nimesema kilo 1.5 kwa wale kuku wadogo wadogo na kilo 2 kwa wale wakubwa

3.Chotara wa miezi miwili bei yake sokoni ni sh ngap?

๐Ÿ‘‰๐ŸฝBei ni 10,000-11,000 Kutegemeana na soko unalolihudumia

Habari yako mkuu hivi hii cpf naweza kuchanganya chakula kwa ajili ya kuku wa kienyeji๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐ŸฝNdio unaweza kutumia CFP k...
24/07/2026

Habari yako mkuu hivi hii cpf naweza kuchanganya chakula kwa ajili ya kuku wa kienyeji

๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ

Ndio unaweza kutumia CFP kuchanganya chakula cha kuku wa kienyeji

Formula za kutumia ni zile zile zinazotumika kuandaa chakula cha kuku chotara

CFP ni virutubisho vinavyotumika kuchanganya chakula cha kuku chotara kuanzia siku 1 mpaka unapowauza au wanapoanza kutaga ukiwa na CFP unahitaji mahindi paraza, pumba za mahindi, mashudu ya alizeti na soya kavu kukamilisha chakula kamili kitakachokupa matokeo mazuri ๐Ÿ”ฅ

Zingatia CFP inatumika kilo 5 kwenye chakula kilo 100 au kilo 25 kwenye chakula kilo 500

Kwa vifaranga kuanzia siku 1 mpaka wiki 3 tunatumia soya tu, kuanzia siku 25 na kuendelea unaweza kutumia uduvi au dagaa

Zingatia chaguo namba moja ni soya kwasababu ya ubora wake na imeshaandaliwa kwa ajili ya kutumika kwenye chakula cha kuku

Zingatia kwa vifaranga pekee ndio tunaweka mafuta ya mboga

Zingatia kwa kuku chotara au kienyeji wanaotaga kwenye formula yao ndio tunaweka chokaa kwasababu kuku Wanaotaga wanahitaji calcium kwa wingi ili kutengeneza Ganda la yai

Moshi Agrovet kiongozi Mimi ni mgeni kwenye ufugaji hivi hiyo cfp   ndo stater au maana sielewi๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐ŸฝCFP sio starter n...
24/07/2026

Moshi Agrovet kiongozi Mimi ni mgeni kwenye ufugaji hivi hiyo cfp ndo stater au maana sielewi

๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ
CFP sio starter ni virutubisho vinavyotumika kuchanganya chakula cha kuku chotara

Chakula hicho kinaweza kuwa starter kwa ajili ya vifaranga, grower kwa ajili ya kuku wanaokua au kikawa ni chakula cha kuku wanaotaga

Kuku hapo namaanisha kuku chotara, maana yake kwenye kila hatua Kuna CFP yake hivyo ipo CFP ya vifaranga, ipo CFP ya kuku wanaokua na ipo CFP ya kuku wanaotaga

Kwahiyo unapochanganya chakula unahitaji CFP na vitu vingine vichache k**a hivi kukamilisha chakula kamili mfano unataka kuchanganya chakula cha vifaranga kilo 100 utaweka hivi

Mahindi paraza kilo 52
Soya kavu kilo 32
Mashudu ya alizeti kilo 9
Mafuta ya mboga kilo 2 [Lita 2.26]
CFP ya vifaranga kilo 5

Unaweza kujiuliza mbona vitu ni vichache hakuna premix, dcp au micro ingredients yoyote unayoifahamu

Jibu lake ni CFP ambayo ni muunganiko wa virutubisho vidogo vidogo vinavyotumika kuchanganya chakula cha kuku kwahiyo ndani ya CFP Kuna hizo premix, dcp... ukitumia CFP huhitaji kuweka hizo ingredients ndogo ndogo

Summary

๐Ÿ‘‰๐ŸฝCFP sio starter Wala sio chakula kamili

๐Ÿ‘‰๐ŸฝCFP ni virutubisho vidogo vidogo vinavyotumika kuchanganya chakula cha kuku

CFP kwasasa zinapatikana hapa

1.Dodoma, Majengo Sokoni pembeni ya CRDB MAJENGO

Mawasiliano ๐ŸŽ๐Ÿ•๐Ÿ“๐Ÿ๐Ÿ—๐Ÿ๐Ÿ๐Ÿ๐Ÿ‘๐Ÿ ๐š๐ฎ ๐ŸŽ๐Ÿ•๐Ÿ๐Ÿ– ๐Ÿ๐Ÿ—๐Ÿ ๐Ÿ‘๐Ÿ•๐Ÿ–

2.Dar es salaam, Ubungo

Mawasiliano ๐Ÿฌ๐Ÿณ๐Ÿญ๐Ÿฑ๐Ÿฒ๐Ÿฒ๐Ÿฌ๐Ÿณ๐Ÿณ๐Ÿญ

3.Iringa mjini

Mawasiliano ๐ŸŽ๐Ÿ•๐Ÿ“๐Ÿ‘ ๐Ÿ‘๐Ÿ๐Ÿ“ ๐Ÿ๐Ÿ๐Ÿ

4.Arusha mjini

Mawasiliano ๐ŸŽ๐Ÿ•๐Ÿ—๐ŸŽ ๐Ÿ•๐Ÿ—๐Ÿ— ๐Ÿ•๐Ÿ”๐Ÿ”

Ninavyojua mahindi paraza ni Yale mahindi ya kande ambayo yanakuwa yamekobolewa ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐ŸฝAsante kwa maoni yako sasa jambo...
22/07/2026

Ninavyojua mahindi paraza ni Yale mahindi ya kande ambayo yanakuwa yamekobolewa

๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ

Asante kwa maoni yako sasa jambo la msingi kuhusu mahindi ni SAIZI yake ili yaweze kuliwa na vifaranga, hayo mahindi ya makande vifaranga hawawezi kuyala punje zake ni kubwa sana

Nikupe mfano wa chakula cha vifaranga kuanzia siku 1

Mahindi paraza kilo 52
Soya kavu kilo 32
Mashudu ya alizeti kilo 9
Mafuta ya mboga kilo 2
CFP ya vifaranga kilo 5

Jumla kilo 100, gharama yake ni 141,000

Kwahiyo Nenda kwenye mashine za kuchanganya chakula cha kuku ulizia mahindi kwa ajili ya vifaranga utapata SAIZI husika

K**a ulipo hakuna mashine za kuchanganya chakula cha kuku au zipo mbali sana basi nenda kwenye mashine za kusaga Unga wa ugali halafu yasage hayo mahindi kiufupi saga Dona [usiyakoboe]

ZINGATIA SAIZI YA MAHINDI ILI VIFARANGA WAWEZE KUYALA

๐Ÿ‘‰๐ŸฝPicha ni mahindi yaliyovunjwa tunayotumia kwa ajili ya vifaranga wetu, nilitaka kusema mahindi paraza ila itoshe kusema ni mahindi yaliyovunjwa hapo tumetumia chekeche ya vifaranga

Tunatumia Mashine ya kuchanganya chakula cha kuku ile kubwa ya tani moja inakuja na grinder pamoja na mixer

Kuagiza CFP tupigie 0752 912132
Tunapatikana Dodoma Majengo Sokoni

Address

Fatina/Majengo Soko Kuu Karibu Na CRDB
Dodoma

Opening Hours

Monday 07:00 - 19:00
Tuesday 07:00 - 19:00
Wednesday 07:00 - 19:00
Thursday 07:00 - 19:00
Friday 07:00 - 19:00
Saturday 07:00 - 19:00
Sunday 09:00 - 16:00

Telephone

+255659632332

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Moshi Agrovet posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Moshi Agrovet:

Shortcuts

Share