Mr Business Poultry Farm

Mr Business Poultry Farm Tajirika kupitia ufugaji wa kuku, kwa kujipatia elimu na ushauri bora wa namna ya kujipatia kipato...

🌱 Kila mbegu inapopandwa, kuna ndoto inapandwa pia.Safari ya mafanikio inaanza kwa kujifunza, kufanya kazi kwa bidii, na...
19/05/2026

🌱 Kila mbegu inapopandwa, kuna ndoto inapandwa pia.

Safari ya mafanikio inaanza kwa kujifunza, kufanya kazi kwa bidii, na kuwa na subira. Leo tunakuza siyo tu mimea au mifugo, bali tunajenga kesho bora kwa vijana na jamii yetu💚🐔🌾

Usikate tamaa na ulipoanzia… matokeo makubwa huanza na hatua ndogo.

Endelea kujifunza, endelea kukua, mafanikio yanakuja! ✨






Huduma zetu ni hakika na halisi ...tutakupa huduma za kitabibu na ushauri...
16/05/2026

Huduma zetu ni hakika na halisi ...tutakupa huduma za kitabibu na ushauri...

🐓Ugonjwa wa Gumboro kwa Kuku🦆GUMBORO NINI?Gumboro ni ugonjwa hatari wa virusi kwa kuku unaoshambulia kinga ya mwili na k...
12/05/2026

🐓Ugonjwa wa Gumboro kwa Kuku🦆

GUMBORO NINI?

Gumboro ni ugonjwa hatari wa virusi kwa kuku unaoshambulia kinga ya mwili na kusababisha vifo vya haraka hasa kwa vifaranga.

Hakuna dawa maalum ya kuutibu, hivyo chanjo na usafi wa banda ndiyo kinga bora. Linda mifugo yako mapema.”

✅️Ugonjwa huu hushambulia kinga ya mwili wa kuku na kuwafanya kuwa dhaifu dhidi ya magonjwa mengine. Mara nyingi huwapata kuku wenye umri wa wiki 3 hadi 6.

DALILI ZA UGONJWA WA GUMBORO
👉Kuku kuwa dhaifu na kukaa sehemu moja

👉Kukosa hamu ya kula

👉Kuharisha choo cheupe au cha maji

👉Manyoya kusimama na kuonekana. kuchoka

👉Kutetemeka mwili

👉Kunywa maji mengi kuliko kawaida

👉Vifo vya ghafla kwa idadi kubwa ndani ya muda mfupi

CHANZO CHA UGONJWA

🐓Ugonjwa huu husababishwa na virusi vinavyoenea kupitia:

🐓Kinyesi cha kuku wagonjwa

🐓Maji au chakula kilichochafuliwa

🐓Viatu, vifaa au watu kutoka banda moja kwenda jingine

🐓Banda chafu lisilozingatia usafi

TIBA YA GUMBORO
Hakuna dawa maalum ya kuua virusi vya Gumboro. Kuku hupewa huduma za kuwasaidia tu k**a:

👍Kuwapa maji safi yenye vitamins na glucose

👍Kupunguza msongamano bandani

👍Kuweka banda safi na lenye hewa nzuri

👍Kutumia dawa za kuzuia maambukizi mengine ya bakteria kwa ushauri wa daktari wa mifugo

NAMNA YA KUJIKINGA NA GUMBORO

1️⃣Chanjo ya Gumboro itolewe kwa wakati sahihi

2️⃣Kudumisha usafi wa banda kila siku
3️⃣Kutenga kuku wagonjwa na wazima

4️⃣Kuzuia watu wengi kuingia bandani hovyo

5️⃣Kusafisha vifaa vya chakula na maji mara kwa mara

6️⃣Kununua vifaranga kutoka sehemu zinazoaminika

MUHIMU KWA WAFUGAJI

⚪️Gumboro inaweza kusababisha hasara kubwa sana kwa wafugaji wa kuku wa nyama (broiler) na kuku wa mayai. Chanjo na usafi ndiyo kinga kubwa dhidi ya ugonjwa huu.

KARIBU KWA HUDUMA ZA VIFARANGA, VYAKULA VYA KUKU, VIFAA VYA KUKU NA USHAURI WA TIBA KWA KUKU..

MAWASILIANO;
+255 742 922 995
+255 682 218 768

23/03/2026
23/03/2026

Je, unalisha kuku au unavuna faida? 🥚💰
Acha kupoteza chakula na kupambana na magonjwa ya chini! Kwa Battery Cages zetu:

✅ Mayai 95% kila siku.
✅ Chakula hakipotei (Zero wastage).
✅ Banda safi muda wote.

Fuga kisasa, vuna kitalamu! 🚀
📍 Kibaha, Pwani
📞 Simu: 0742 922 995

23/03/2026

🥚 JE, UNATAKA KUPATA MAYAI 90% -95% KILA SIKU NA KUPUNGUZA GHARAMA ZA CHAKULA? 🥚

Mfugaji makini, unajua siri ya kupata faida kubwa kwenye kuku wa mayai (layers)? Siri haipo kwenye idadi ya kuku tu, bali ipo kwenye MFUMO WA UFUGAJI.

Kwanini utumie Cages (Mabanda ya Kisasa) badala ya kufugia chini?

✅ Huokoa Chakula (Zero Wastage): Kuku hawezi kumwaga chakula wala kukivuruga. Kila punje ya chakula inageuka kuwa yai!

✅ Usafi na Kinga ya Magonjwa: Kinyesi kinaanguka chini mbali na kuku. Hii inakata mazalia ya wadudu na magonjwa k**a Coccidiosis (Kuhara damu).

✅ Mayai Safi na Salama: Mayai yanashuka yenyewe kwenye sehemu maalum. Hakuna mayai kupasuka, kuliwa na kuku, au kuchafuliwa na kinyesi.

✅ Usimamizi Rahisi: Ni rahisi kumtambua kuku asiyetaga, mgonjwa, au anayekula bila kutoa matokeo. Unahifadhi muda na nguvu kazi!

✅ Nafasi Ndogo, Kuku Wengi: Cage inakuwezesha kufuga kuku wengi kwenye eneo dogo sana kwa sababu ya mfumo wa ghorofa (tiers).

🚀 BORESHA BANDA LAKO LEO! 🚀
Tunatoa Cages bora na imara (Galvanized) ambazo hazishiki kutu na zinadumu kwa miaka mingi.

📦 ZINAKUJA NA:

Mifumo ya maji ya Automatic (Ni***es).

Sehemu za kulia chakula (Feeders).

Rahisi kufunga na kusafisha.

📍 Tupo: Kibaha, Pwani
📞 Wasiliana nasi sasa: +255 742922995,
💬 Tuma ujumbe (DM) kwa ushauri wa bure wa jinsi ya kuanza!

Fuga kisasa, vuna faida! 📈 MFUGAJI UKISHINDWA UJAAMUA

Address

Dar Es Salaam
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00
Sunday 09:00 - 17:00

Telephone

+255682218768

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mr Business Poultry Farm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share

Category