14/08/2026
Unafungua kesi alafu wewe ndo unalazimishwa ulete mashahidi sasa umefungua ya nini hii jamuhuri au takataka
Leo Agosti 14, 2026
Jana tuliishia part 242 so leo tunaendelea na -;
Part 243
Imepigwa high Court ila tofauti na siku nyingine leo kaipiga Mwakasala
Majaji wameingia,
Karani wa Mahak**a anasimama kusoma namba ya shauri.
Mawakili wa Serikali wamekaa k**a hawana shahidi leo maana hawaeleweki.
Crimina 19605/2025 Jamhuri dhidi ya Lissu. kisha karani anakaa chini.
Iwapendeze naitwa Ajuaye, Ignas mwinuka, Thawabu Issa, Cattbert Mbilinyi na Winniwa Kasawa na Msh*takiwa yupo kizimbani.
Na shauri limekuja kwa ajili ya kusikilizwa.
Waheshimiwa Majaji shahidi tuliyemuandaa leo amepata dharula kwahiyo ameenda muhimbili kwahiyo tunaomba ahirisho hadi jumatatu tutaleta mashahidi wetu wote.
Mheshimiwa Tundu Lissu anacheka tu. Kile kicheko cha kusema hivi haya majitu yana akili kweli? Unakijua kile kicheko cha hasira na cha kusema wewe ni mpumbavu nini?
Watu wanasonya sana.
Majaji wanaandika kidogo hapa.
Ngoja tusubiri Mheshimiwa Lissu anasemaje.
Amesimama anasema mimi niko tayari kuendelea na kesi le, ninapinga ombi la kuahirisha kesi hii kutokana na sababu zilizotolewa na wakili wa serikali.
Kulikuwa na amri ambayo mlitoa mwaka jana kwamba upande wa Mash*taka ulete mashahidi wasiopungua wawili kila siku kesi hii inaposikilizwa. Na hii amri mmeirudia juzi ukiachia jana, siku ya Jumatano na mmeirudia jana.
Upande wa mash*taka walete mashahidi wengi sasa hautekelezi amri za Mahak**a kwasababu wanaamini nyie Majaji mmeshindwa kuwachukulia hatua na wanajua Mahak**a itawakubalia.
Mimi kusema maneno haya sio kitu chepesi sana lakini naamini hamjachukua hatua kabisa. Kila siku mnawapa maelekezo wao wanapuuza. Wanatuaminisha hapa na Dunia kuwa wanaweza kufanya lolote.
Sasa kwa vile jana mlirudia tena kwamba walete mashahidi na hawajaleta.
Msikubali Mahak**a kuu ya Tanzania ikageuzwa k**a ile Mahak**a iliyomuhukumu Jomo Kenyatta. Mahak**a ya Jaji Thucker ilisemwa kule London kuwa iliwakubalia kila kitu kilichoombwa na Mawakili wa serikali.
Msije mkafanywa hivyo, msiwakubalie mambo yasiyokuwa na msingi kwanini hawako tayari kuheshimu maamuzi ya Mahak**a.???
Mimi naamini wamekata pumzi na huyu mbaya wao aendelee kusota gerezani na wao waendelee kuvuta posho za Serikali, Msikubali kugeuzwa k**a hiyo mahak**a niliyoisema.
Again for the record hii ndio kesi kubwa kuliko zote katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hivyo hii mahak**a inapaswa kuonekana ikisimamia amri zake ili kulinda hadhi ya Mahak**a.
Hatutembelei kwenye njia ambayo haijafagilia. 1970, Grey Likungu Mataka kesi ya ugaidi ya kwanza.
Kesi ilichukua miezi sita kuanzia Mahak**a kuu hadi ile ya rufani, njia hii ikasafishwa vizuri zaidi Mwaka 1982 Khatibu Gandi na wenzake katika Mahak**a Kuu chumba hiki hiki kesi ilichukua mwaka 1 na siku 17.
Na haya ninayosema yapo kwenye record ya hizo kesi mbili kwahiyo mnayo mifano. Leo ni siku ya 493 yani mwaka 1 na miezi 4 hatujamaliza.
Nikija kusema aitwe Samia Suluhu Hassan si itachukua miaka 5 mtastaafu bila kesi hii kuitwa.
Maana nataka Philip Mpango, Kassim Majali na IGP nikisema waje kesi si haitaitwa milele? Jitahidini hii Mahak**a isiwe Kangaroo Court.
Nimemaliza.
Anasimama Ajuaye, Wakili wa Serikali tumemsikia mwenzetu alichoongea lakini mashahidi ni wanadamu na kwakuwa wanadamu changamoto inaweza kutokea muda wowote na kwa binadamu yeyote.
Sisi upande wa mash*taka tunakili kuwa ni kweli bado tuna mashahidi wengi lakini sio lazima tulete wote, pengine ni shahidi wa mwisho na ndio huyo tunayemtegemea sasa hakuna namna kifungu cha 265 CPA.
Tunaomba Mahak**a yenu iahirishe shauri hili mpaka Jumatatu na tutaleta mashahidi wote waliobakia, wote kabisa waliobakia na itakuwa ndani ya session hii na kikao hiki kilichopangwa.
Part 244 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.