Mtu wa Mungu

Mtu wa Mungu I GREET EVERY BODY IN THE NAME OF YESHUAH HAMASHIACH (JESUS CHRIST) OUR ADONAY ELOH.

MY NAME IS RENATUS BAVUMA FROM TANZANIA 🇹🇿 EAST AFRICA;

AM HERE FOR THE GREAT CAMISSION OF ALMIGHTY GOD

WICH IS TO TEACH AND TO PREACH THE GOSPEL OF JESUS.

NENO LA WEEK HII Ndugu na Dada Katika Mwili wa Kristo,  Shavua Tov "Juma hili Jema"; Mimi Mtu wa Mungu,  Nakutakia Week ...
23/08/2026

NENO LA WEEK HII

Ndugu na Dada Katika Mwili wa Kristo, Shavua Tov "Juma hili Jema";
Mimi Mtu wa Mungu, Nakutakia Week Njema Iliyojaa Ulinzi wa Mungu kwako, Uzima wa Mungu kwako, Uhai wa Mungu kwako, Afya Njema Katika roho yako, nafsi yako, na mwli wako:

Leo ni Siku ya 14 Tangu tulipoanza
{"Safari ya Siku 40 na Mfalme"} ADONAI ELOHEINU, Amekuwa Mwema kwetu, na Ameendelea Kututia Nguvu za "Kuomba na Kufunga" Hakika, Jina lake Litukuzwe Katika Anga la Uweza wake.

"Neno la Week Hii"

Neno letu la Week Hii, Linatoka Katika Kitabu cha (Tehillim 27:4)
Au
(Zaburi 27:4)

Nukuu: Neno Moja Nimelitaka kwa ADONAI, Nalo Ndilo Nitakalolitafuta, Nikae Nyumbani mwa ADONAI Siku zote za maisha yangu, Niutazame Uzuri wa ADONAI, Na Kutafakari Hekaluni mwake.

Neno la Kiebrania Linatumika kwenye Mstari huu ni hili; {"Achat Sha'alti Me'et YHWH Otah Avakeish"} yaani Neno moja nimelitaka kwa ADONAI!

▪︎ Mfalme Daudi ndiye aliye sema akimaanisha kwamba, Wakati wa Vita, wakati shida, wakati wa Changamoto za Maisha, Yeye Hutaka Neno moja tu kwa Mungu, Kukaa Nyumba mwake!

▪︎ Daudi, Hakutaka fedha, wala Ushindi dhidi ya adui zake, Yeye Alitaka Akae pamoja na Mungu tu:

Je! Wewe na Mimi, Changamoto za maisha, zinapotuzidia tunataka neno gani kwa ADONAI ELOHEINU?

"Vitu 3 vya Kuzingatia"

â™§ {Lachazot B'Noam YHWH}
Niutazame Uzuri wako ADONAI, ni kweli dunia ina mazuri yake, Lakini ya muda mfupi:
Maana, Uzuri wa ADONAI ELOHEINU Unadumu, ni wa Milele na Milele.

â™§ Neno Moja Nimelitaka kwa ADONAI, Nalo Ndilo "Ninalolitafuta", Nikae Nyumbani mwa ADONAI Siku zote za maisha yangu.

â™§ Nitafakari Hekaluni mwako ADONAI.

Ndugu na Dada Katika Mwili wa Kristo, Hebu Tazama, Angalia, ili Uone Uso Mungu, Wema wa Mungu, Baraka za Mungu, na Miujiza ya Kupita kawaida;
Ni Katika Jina la Yesu Kristo wa Nazareth, Mwana wa Mungu aliye Hai.

ISRAEL DOCTORS  MADE MADICAL HOSTORY IN THE WORLD For the Glory of Almighty ADONAI ELOHEINU,  Patients  with recurrent D...
21/08/2026

ISRAEL DOCTORS MADE MADICAL HOSTORY IN THE WORLD

For the Glory of Almighty ADONAI ELOHEINU, Patients with recurrent Disease currently have very Limeted treatment Options - Prof. Aron Popovtzer, Director of the Sharett Institute of Oncology

Hadassah - University Medical Centre Announced Success in Applying a new treatment for recurrent Aggressive Brain Tumors Using Alpha DaRT radiation technology.

The treatment uses bio - efficient Alpha Particles Placed near the tumor from two different Vectors to deliver Concentrated radiation whele minimising damage to surrounding Brain tissue.

The Procedure marks the first use of the treatment in ISRAEL, Providing a local, Precise, and Minimally invasive treatment without the need for extensive Brain surgery.

Glory be to Yeshuah haMashiach

FAMILIA YA ISRAEL Ndugu na Dada Katika Mwili wa Kristo,  Shabbat Shalom Shalom!Kwa Unyenyekevu Mkubwa,  Nimeona vyema "N...
21/08/2026

FAMILIA YA ISRAEL

Ndugu na Dada Katika Mwili wa Kristo, Shabbat Shalom Shalom!

Kwa Unyenyekevu Mkubwa, Nimeona vyema "Nikudadavulie" juu ISRAEL na Chimbuko lake k**a familia, ili tujue wote ya kuwa Taifa la ISRAEL lilitokea wapi.

Chini hapa, Nimeweka "Jedwari" ili itusaidie Kuelewa kile nacholenga tukijue wote kwa Umoja wetu!

KUTOKA IBRAHIM MPAKA YAKOBO

FAMILIA YA SRAEL

> Leah
> Ibrahim
> Rebecca
> Sarah
> Issac
> Rachel
> Jakobo

Hawa Ndiyo Ma-Baba, na hawa Ndiyo Mama waliozaa familia ya ISRAEL;

Hata hivyo, ili kuelewa kwa Usahihi, Unaposoma Jedwari hili, Soma toka Upande wa kulia, kwenda upande wa kushoto!
Ndivyo ilivyo andikwa kwa Lugha ya Kiebrania, Jitahidi kufanya hivyo ili tuelewe pamoja kwa Umoja katika Jina la Yesu Kristo wa Nazareth Mwana wa Mungu aliye Hai.

🇮🇱 BARAKA ZA MUNGU KWA ISRAEL 🇮🇱 Ndugu na Dada Katika Mwili wa Kristo Shalom kwako Shalom!Leo ikiwa ni Siku ya 6 ya Juma...
21/08/2026

🇮🇱 BARAKA ZA MUNGU KWA ISRAEL 🇮🇱

Ndugu na Dada Katika Mwili wa Kristo Shalom kwako Shalom!

Leo ikiwa ni Siku ya 6 ya Juma hili, Hebu tuchukue Dakika Chache kwa ajili ya "Kutamka Amani" kwa ISRAEL,
N'na, "Kutamka Baraka" kwa Yerusalimu na watu wake;

ISRAEL, Ni Nchi Takatifu ya "ADONAI ELOHEINU" Muumba wa Mbingu na Dunia;
Nataka tujue, ISRAEL Ni Taifa Lililochaguliwa na Mungu Mwenyezi, kwa Utashi wake Mwenyewe!

ASEMAVYO MUNGU JUU YA ISRAEL

Kwa njia ya Neno lake Takatifu, Liitwalo Biblia, Mungu Anasema!

[6] Kwa maana wewe U Taifa Takatifu kwa ADONAI, ELOHEINU wako; ADONAI ELOHEINU wako, "Amekuchagua" kuwa Watu wake HASA, zaidi ya mataifa yote walioko juu ya uso wa Nchi.

[7] ADONAI hakuwapenda ninyi, wala hakuwachagua ninyi, kwa sababu mlikuwa wengi kuliko mataifa yote, maana "mlikuwa wachache" kuliko watu wote;

[8] bali kwa sababu ADONAI "Anawapenda", na kwa sababu "Alitaka kuutimiza" Uapo wake aliowaapia Baba zenu, Ndiyo Sababu "Akawatoa" kwa mkono wa Nguvu, "Akawakomboa" katika nyumba ya utumwa, katika mkono wa Farao, mfalme wa Misri.

[9] Basi jueni ya ADONAI, ELOHEINU wenu, Ndiye ELOHEINU; MUNGU Mwaminifu, Ashikaye Agano lake na Rehema zake kwao wampendao, na kushika Amri zake, hata Vizazi elfu;

(Kumbukumbu la Torati 7:6-10)

Bila shaka, Umeona na Kutambua ya kuwa, Mungu Mwenyezi, Yeye Ndiye Aliye Chagua Taifa la ISRAEL kuwa Taifa lake Takatifu, Lakini pia, kuwa "Watu wake HASA" Amesema, zaidi ya mataifa yote walioko juu ya uso wa Nchi.

▪︎ Taifa lake Takatifu,
▪︎ Watu wake HASA.

Kwa Sababu hiyo, Imetupasa Kujua Kuomba kwa ajili ya Amani ya ISRAEL, na Kutamka Baraka kwa ISRAEL, Kadiri tuwezavyo.

AHADI YA MUNGU KWA ISRAEL 🇮🇱

(Mwanzo 12:3) Nukuu:

[3] Mungu anasema!

Nami "Nitawabariki" wakubarikio, naye akulaaniye "Nitamlaani"; na katika wewe {ISRAEL} jamaa zote za dunia "watabarikiwa".

â—‡ Hii ni Ahadi ya Mungu kwa ISRAEL, Lakini pia, ni Ahadi ya Mungu kwa "Wanaobariki" ISRAEL Kwa maneno ya Kutamka, au kwa Mali zao; Anasema, {"Nitawabariki" wakubarikio.}

â—‡ Ahadi ya Pili kwa ISRAEL, Mungu anasema, naye 'Akulaaniye' "Nitamlaani"

Kwa maana hiyo, Uchaguzi ni wa Mimi na wewe;

▪︎ Ukichagua "Kubariki ISRAEL", Mungu wa ISRAEL, "Anakubariki wewe":

▪︎ Ukichagua "Kulaani ISRAEL", Mungu wa ISRAEL "Anakulaani wewe".

Ndugu na Dada Katika Mwili wa Kristo, Ni wakati wa Kufanya Uchaguzi Sahihi ili Kuona Kubarikiwa na Mungu wa ISRAEL. .Ooh, Hallelujah..!!

19/08/2026
TUNAENENDA "KWA IMANI" SI "KUONA"Ndugu na Dada Katika Mwili wa Kristo Shalom kwako Shalom!Nataka tujue,  Mbinguni tunaen...
19/08/2026

TUNAENENDA "KWA IMANI" SI "KUONA"

Ndugu na Dada Katika Mwili wa Kristo Shalom kwako Shalom!

Nataka tujue, Mbinguni tunaenda kwa Imani, Kwa Njia ya Neema, iliyo Katika "Yeshuah haMashiach" (Yesu Kristo)
Kwa kuwa Imenenwa;

(2 Wakorintho 5:7-10) Nukuu:

[7] {Maana 'Tunaenenda' "Kwa Imani" Si "Kwa Kuona".}

Zaidi ya yote, Kila Kitu katika maisha, Kinaanza katika Ulimwengu wa roho, Si katika Ulimwengu wa nyama;
Hii ndiyo Sababu, Kwa nini "Tuenende kwa Imani" na Si kwa Kuona!

â—‡ Elimu huanzia katika Ulimwengu wa roho,

â—‡ Ajira huanzia katika Ulimwengu wa roho,

â—‡ Kazi huanzia katika Ulimwengu wa roho,

â—‡ Baraka huanzia katika Ulimwengu wa roho,

â—‡ Mafanikio huanzia katika Ulimwengu wa roho,

â—‡ Utajiri huanzia katika Ulimwengu wa roho,

â—‡ Hata Umasikini huanzia katika Ulimwengu wa roho,

â—‡ Kushinda au kushindwa, huanzia katika Ulimwengu wa roho pia.

Swali la Msingi:

Wewe na Mimi, tunaona Nini katika Ulimwengu Usioonekana? Ujue, Ulimwengu usio onekana ndio Ulimwengu wa roho.

JE! IMANI NI NINI?

Biblia inasema, Imani Ni kuwa na Hakika ya Mambo yatarajiwayo, N'na ni "Bayana" ya "Mambo yasiyo Onekana";

Ukweli ni kwamba, yapo mahali fulani, ila "Hayaonekani kwa macho ya nyama", Bali, yanaonekana kwa macho ya Imani;

N'na, "Macho ya Imani" huona katika Ulimwengu wa roho,
Kisha, "Huvuta" Kile yanachoona katika Ulimwengu wa roho, maana "Yanauwezo huo wa Kuvuta" vitu katika Ulimwenguwaroho. .Ooh, Hallelujah..!!

[8] Lakini tuna moyo Mkuu; Nasi tunaona ni afadhali kutokuwamo katika mwili, na kukaa pamoja Adonai.

[9] Kwa hiyo, tena, ikiwa tupo hapa, au ikiwa hatupo hapa, twajitahidi Kumpendeza Yeye.

[10] Kwa maana imetupasa sisi sote kudhihirishwa mbele ya Kiti cha Hukumu cha Kristo, ili kila mtu apokee ijara ya mambo aliyotenda kwa mwili, Kadiri alivyotenda, kwamba ni mema au mabaya.

ANGALIZO:

Imetupasa sisi sote Kudhihirishwa mbele ya Kiti cha Hukumu cha Kristo, ili kila mtu apokee ijara ya mambo aliyotenda, kwamba ni mema au mabaya;

Kumbuka:

Biblia inasema, Roho Mwenyewe Hushuhudia Pamoja na roho zetu, ya kuwa Sisi tu watoto wa Mungu; na k**a tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na Kutukizwa pamoja naye.
"Warumi 8:16,17"

NATAKA TUJUE

Ndugu na Dada Katika Mwili wa Kristo, Nataka tujue, Mbinguni tunaenda kwa Imani, kwa njia ya Neema yake "GEULAH" Yeshuah haHamashiach.

▪︎ Imani, inatupa Kuona Kuingia Mbinguni Pamoja na "HaMashiach" (Kristo) Katika Ulimwengu wa roho,

▪︎ Wakati Neema yake "HaMashiach" Inatubeba, na "Kutuingiza kwa Nguvu" za Uweza wake Mwenyewe Yeye aliye Kufa akafufuka toka kwa Wafu..Ooh, Hallelujah..!!

ANGALIA SIKU ZINAKUJA (Yeremea 31:31-34)Ndugu na Dada Katika Mwili wa Kristo Shalom Shalom kwako!Nataka "tudadavue" juu ...
13/08/2026

ANGALIA SIKU ZINAKUJA

(Yeremea 31:31-34)

Ndugu na Dada Katika Mwili wa Kristo Shalom Shalom kwako!

Nataka "tudadavue" juu ya Ahadi ya Mungu kwa watu wake ISRAEL, Lakini pia, Ahadi ya Mungu, kwa watu wake Kanisa la Kristo, au Mwili wa Kristo.

Hivi ndivyo, yanenavyo Maandiko!

[31] Angalia, siku zinakuja, asema ADONAI, Nitakapofanya "Agano Jipya" na Nyumba ya ISRAEL, na Nyumba ya Yuda.

[32] Si kwa mfano wa Agano lile nililofanya na baba zao, katika siku ile nilipowashika mkono, ili kuwatoa katika nchi ya Misri;
ambalo agano langu hilo walilivunja, ingawa nalikuwa Mume kwao, asema ADONAI.

[33] Basi Agano hili ndilo Nitakalofanya na Nyumba ya ISRAEL, baada ya siku zile, asema ADONAI;
Nitatia Sheria yangu ndani yao, na katika mioyo yao Nitaiandika; Nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.

Ndugu na Dada Katika Mwili wa Kristo, Nataka tujue hivi kwamba, Kuna wakati Sisi watu wa Mungu, tunaposoma Torati, tunasema torati Si Maelekezo Mungu kwetu wakati huu;

Kwa nini?

Kwa Sababu tunashindwa kuelewa "Thiolojia" na kuthani ya kuwa Kuna Mistari ya Biblia inawahusu wana wa ISRAEL tu, ila sisi haituhusu Kabisa!

Kitu cha Kuzingatia

Torati haimanishi kuwa ni Vitabu 5 vya Musa kwa wana wa ISRAEL tu;
Bali, Torati Humaanisha kuwa ni "Mafundisho ya Neno la Mungu kwa watu wa Mungu, Lakini pia, torati ni "Maelekezo Mungu", na Kanuni zake kwetua Sisi.

Kumbuka:

Kuna wakati Yeremea, alikuwa akisema na wana wa ISRAEL kwa "Kurudi rudia" juu ya torati, hata hivyo ilikuwa Ngum kwao Kuiishi torati hiyo;

Tazama!

(Yeremea 6:19)

[19] Sikia, Ee Nchi; tazama, nitaleta mabaya juu ya watu hawa, naam, matunda ya mawazo yao, kwa sababu hawakuyasikiliza maneno yangu;
tena kwa habari ya sheria yangu, wameikataa.

(Yeremea 9:13)

[13] Naye ADONAI asema, Ni kwa Sababu wameiacha Sheria yangu niliyoweka mbele yao, wala hawakuitii Sauti yangu, wala kuendenda katika hiyo;

(Yeremea 16:11)

[11] Ndipo utakapowaambia, Ni kwa Sababu baba zenu wameniaacha Mimi, asema ADONAI, na kuwafuata miungu mingine, na kuwatumikia na kuwaabudu, wakaniacha Mimi, wasiishike torati yangu;

Bila shaka, Umeona jinsi wana wa ISRAEL walivyoshindwa kutii Sheria ya ADONAI ELOHEINU wao, na kugeukia miungu mingine na kuiabudu, na kuitumikia, ikawachukizo mbele za ADONAI ELOHEINU wao.

Kwa 'mantiki' hiyo, Mungu Aliposema, Nitatia Sheria yangu ndani yao, Hakumaanisha "Kubadili Agano" la kwanza kuwa Agano Jingine zaidi ya hilo la kwanza;

Bali, Alimaanisha hivi, Kwamba, {"Ataiandika Katika Vibao vya Mioyo yetu"} na Kwamba, Atatia Roho wake Mtakatifu ndani ya roho zetu, ili Roho wake Mtakatifu Aweze Kuziongoza roho zetu Kutii Sheria ya ADONAI na Kuifuta kwa Usahihi.

Tazama:

(Ezekiel 36:27)

[27] Nami nitatia "Roho yangu" ndani yenu, na kuwaendesha katika Sheria zangu, nanyi mtazishika Hukumu zangu, na Kuzitenda.

Ndugu na Dada Katika Mwili wa Kristo, Nataka tujue, Roho Mtakatifu si Mbadala wa Sheria ya ADONAI, Bali Roho wa Mungu, Anatufanya Sisi tuwe "Active" Kutembea katika Sheria zake Mzee wa Siku kwa Usahihi.

Lakini pia, tujue hivi kwamba, "Yeshuah haMashiach" Yeye Ndiye Kitovu cha Agano Jipya wala si vinginevyo;
Ndiyo, Utii wetu huja kwetu kupitia Roho wake Mtakatifu ndani yetu!

Ndiyo, Wokovu wetu pia, Huja kwa "Neema", kwa Njia ya "Imani" iliyo Katika Kristo Yesu.

Hii ndiyo Sababu, Yesu Kristo Ndiye BWANA wa Sabato wala si vinginevyo!

Angalizo:

{Katika Yeremea amesema, Nitatia Sheria yangu ndani yao, na katika mioyo yao Nitaiandika;}

{Na katika Ezekiel amesema, Nami Nitatia roho yangu ndani yenu, ili kuwaendesha katika Sheria zangu, nanyi mweze kuzishika Hukumu zangu na Kuzitenda.}

Ndugu, Hebu Tudumu katika fundisho la Mitume na Katika Ushirika, Huku Tukimega Mkate Nyumba kwa Nyumba;

Ni kwa Jina la Yesu Kristo wa Nazareth, Nakushauri Kumega Mkate mara kwa mara Kadiri inavyowezekana, na kwa Utukufu wa Mzee wa Siku;
Amen tena Amen.

31/07/2026

Address

Mbezi Louis
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mtu wa Mungu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mtu wa Mungu:

Shortcuts

Share

Category