23/08/2026
NENO LA WEEK HII
Ndugu na Dada Katika Mwili wa Kristo, Shavua Tov "Juma hili Jema";
Mimi Mtu wa Mungu, Nakutakia Week Njema Iliyojaa Ulinzi wa Mungu kwako, Uzima wa Mungu kwako, Uhai wa Mungu kwako, Afya Njema Katika roho yako, nafsi yako, na mwli wako:
Leo ni Siku ya 14 Tangu tulipoanza
{"Safari ya Siku 40 na Mfalme"} ADONAI ELOHEINU, Amekuwa Mwema kwetu, na Ameendelea Kututia Nguvu za "Kuomba na Kufunga" Hakika, Jina lake Litukuzwe Katika Anga la Uweza wake.
"Neno la Week Hii"
Neno letu la Week Hii, Linatoka Katika Kitabu cha (Tehillim 27:4)
Au
(Zaburi 27:4)
Nukuu: Neno Moja Nimelitaka kwa ADONAI, Nalo Ndilo Nitakalolitafuta, Nikae Nyumbani mwa ADONAI Siku zote za maisha yangu, Niutazame Uzuri wa ADONAI, Na Kutafakari Hekaluni mwake.
Neno la Kiebrania Linatumika kwenye Mstari huu ni hili; {"Achat Sha'alti Me'et YHWH Otah Avakeish"} yaani Neno moja nimelitaka kwa ADONAI!
▪︎ Mfalme Daudi ndiye aliye sema akimaanisha kwamba, Wakati wa Vita, wakati shida, wakati wa Changamoto za Maisha, Yeye Hutaka Neno moja tu kwa Mungu, Kukaa Nyumba mwake!
▪︎ Daudi, Hakutaka fedha, wala Ushindi dhidi ya adui zake, Yeye Alitaka Akae pamoja na Mungu tu:
Je! Wewe na Mimi, Changamoto za maisha, zinapotuzidia tunataka neno gani kwa ADONAI ELOHEINU?
"Vitu 3 vya Kuzingatia"
â™§ {Lachazot B'Noam YHWH}
Niutazame Uzuri wako ADONAI, ni kweli dunia ina mazuri yake, Lakini ya muda mfupi:
Maana, Uzuri wa ADONAI ELOHEINU Unadumu, ni wa Milele na Milele.
â™§ Neno Moja Nimelitaka kwa ADONAI, Nalo Ndilo "Ninalolitafuta", Nikae Nyumbani mwa ADONAI Siku zote za maisha yangu.
â™§ Nitafakari Hekaluni mwako ADONAI.
Ndugu na Dada Katika Mwili wa Kristo, Hebu Tazama, Angalia, ili Uone Uso Mungu, Wema wa Mungu, Baraka za Mungu, na Miujiza ya Kupita kawaida;
Ni Katika Jina la Yesu Kristo wa Nazareth, Mwana wa Mungu aliye Hai.